Jumamosi, 15 Machi 2014

SARUFI ZA KISWAHILI 2

TABIA ZA VITENZI VYA KISWAHILI
            Vitenzi vya Kiswahili huwa na tabia tofauti tofauti zinazotokana na dhima za mofimu ambazo hupachikwa katika vitenzi hivyo, hivyo kulingana na dhima za mofimu, vitenzi vya Kiswahili huwa na tabia zifuatazo:-
       I.            Kutambulisha nafsi. Mfano:- Anayesoma
    II.            Kutambulisha tendo. Mfano:- Cheza, Lima, Imba n.k.
 III.            Kutambulisha wakati. Mfano:- Ulikuja
 IV.            Kutambulisha hali ya uyakinishi na ukanushi. Mfano:- Anacheka – Hacheki
    V.            Kutambulisha kauli mbalimbali za tendo. Mfano:- cheza-chezwa-chezewa-chezeka n.k.
 VI.            Kutambulisha hali ya tendo. Mfano:-Huimba, Amekula.
VII.            Kuonesha urejeshi wa mtenda, mtendwa na mtendewa ambao hujidhihirisha katika ngeli ya nomino iliyotajwa kwa kuzingatia upatanisho wa kisarufi. Urejeshi huo ni wa O-rejeshi. Katika urejeshi huo vitenzi hubeba viambishi ngeli vya –O- isipokuwa kama nomino ni ya ngeli ya kwanza umoja  ambapo hutumia –e- badala ya –O-.
Mfano:-
NGELI
KIAMBISHI CHA O- REJESHI
MFANO
A-WA
-YE- na –O-
Aliyepiga / Waliokuja
U-I
-O- na –YO-
Uliokatwa / Iliyokatwa
LI-YA
-LO- na –YO-
Lililochanika / Yaliyochanika
KI-VI
-CHO- na –VYO-
Kilichovunjika / Vilivyovunjika
I-ZI
-YO- na –ZO-
Iliyofungwa / Zilizofungwa
U-ZI
-O- na -ZO
Uliokatika / Zilizokatika
U-YA
-O- na –ZO-
Ulionipata / Yaliyonipata
KU
-KO-
Kulikotokea
PA-MU-KU
PO-MO-KO
Pale alipoingia / Mule alimotokea / Kule alikofunga




ZOEZI
1.      Fafanua dhana ya sarufi kisha eleza tanzu zinazoijenga.
2.      Eleza umuhimu wa kujifunza sarufi ya Kiswahili.
3.      Onesha tofauti iliyopo kati ya irabu na konsonanti.
4.      Eleza maana ya silabi na uoneshe kwa mifano miundo mitano ya Silabi za Kiswahili.
5.      Nini maana ya mofimu? Fafanua aina zake.
6.      Bainisha dhima za kila mofimu katika maneno yafuatayo:-
a.       Anakula
b.      Waliokutafuta
c.       Tulipokukosa
d.      Nikikukumbuka
e.       Aliyempigia
f.       Hakufika
g.      Huimba
h.      Mnavyopendana
i.        Amemtukana
j.        Ungelifika
7.      Nini maana ya uambishaji na mnyumbulkiko wa maneno? Onesha jinsi dhana hizo zinavyochangia kukuza lugha.
8.      Eleza kauli mbalimbali za vitenzi vya lugha ya Kiswahili.
9.      Pachika viambishi ngeli vya O- rejeshi katika vitenzi vifuatavyo ukibainisha umoja na uwingi:-
a.       Chura amekufa
b.      Kitabu kimechanika
c.       Meza imevunjika
d.      Daftari limechanika
e.       Simu imeita
f.       Ameingia mahali humu
g.      Amepitia pale
h.      Imevunjiwa kule


10.   
A.    Neno
Ni silabi au mkusanyiko wa silabi zinazotamkwa au kuandikwa ambazo huwa na maana (maana yaweza kuwa ni ya kileksika au kisarufi).

AINA ZA MANENO

1.      NOMINO
Ni aina ya neno ambalo hutaja mtu, kitu, mahali, hali na kitendo. Mfano; Mwajuma, Kalamu, Mwanza, Udakitari, Kulima n.k.

Aina za nomino:
·         Nomino za pekee: Nomino za pekee hutaja na kutambulisha nomino mahsusi
na za kipekee. Yaani kuwa kitu ni hicho na wala si chengine chochote. Hizi ni nomino zinazohusisha majina kama vile ya watu, nchi, miji, mito, milima,maziwa na bahari. Herufi za kwanza za nomono za pekee huwa kubwa hata kamanomino hizi zinapatikana katikati ya sentensi. Mfano; baba, Asha, Tanzania, Dodoma, Kilimanjaro, Victoria n.k

·         Nomino za jamii: Hizi kwa jina jengine huitwa nomino za jumla. Nomino hizihazibainishi wazi wazi vitu ambavyo habari zake zinatolewa. Kwa mfano ikiwa nimtu, mahsusi hatambuliwi. Haituambii kama ni Kelvin, Tuafu ama Zawadi.Ikiwani ziwa halitambuliwi kama ni Michigan , Victoria au Nyasa, yaani hutaja vitubila kutaja umahsusi wake kama ilivyo katika nomino za pekee. Hizizinapoandikwa si lazima zianze kwa herufi kubwa isipokuwa zimetumiwamwanzoni mwa sentensi au zimetumika kama anuani ya kutajia kitu kama vileMkuu wa Sheria. Katika mfano huu ‘sheria’ kwa kawaida ni nomino ya kawaida,lakini hapa inaanza kwa herufi kubwa kwani inataja anuwani ya kipekee. Mfano wa nomino za kawaida ni; Mwanafunzi, Mwalimu, Mnyama, Mtazamaji, Askari n.k

·         Nomino za kawaida: Kundi hili la nomino hutumia kigezo cha uwezekano wakuhesabika kuziainisha. Hapa tunatofautisha kati ya nomino zinazowakilisha vitu vinavyohesabika kwa upande mmoja, na vile visivyohesabika kwa upande mwengine. Nomino ya vitu vinavyohesabika vitanda, nyumba, vikombe vitabu kadahlika. Zile zisizohesabika hurejelea vitu ambavyo hutokea kwa wingi na haviwezi kugawika, kwa mfano maji, mate, makamasi, maziwa, moshi, mafuta. Aghlabu nomino hizo huwa sawa katika umoja na wingi.

·         Nomino za kitenzi jina: Hizi ni nomino zinazohusu vitenzi . Huundwa kwa kuongezwa kiambishi {ku-} cha unominishaji kwenye mzizi wa kitenzi cha kitendo halisi ili kukifanya kiwe nomino. Mfano; Kulima, Kucheza, Kuimba n.k

·         Nomino dhahania: Hizi ni nomino ambazo hurejelea vitu vinavyoweza kuhusika na mwanaadamu kupitia milango ya hisia kama macho, mapua, masikio vidole na ulimi- yaani vitu ambavyo haviwezi kushikika, kuonekana, na kuonjeka. Mfano; Vita, Njaa, Ugonjwa, Shetani, Mungu n.k

2. Vivumishi
·         Ni maneno ambayohutoa ufafanuzi au maelezo ya ziada kuhusu jina ili kuitambulisha vyema.
Aina za vivumishi.
·         Vivumishi vya sifa: hutoa sifa za nomino /kiwakilishi cha nomino. Sifa hizi huweza kuwa nzuri, mbaya au yoyote ile.Mfano; mzuri, mbaya, mrembo n.k
·         Vivumishi vya idadi: vinaweza kujitokeza katika aina tatu ndogondogo.Vivumishivya aina hii hutoa taarifa kuhusu idadi ya nomino ambazo kiwango chakekimetajwa. Mfano; wawili, watano, wengi, wachache n.k
·         Vivumishi vya kumiliki: Ni vivumishi vinavyoonesha kuwa kitu fulani kina milikiwa na mtu au kitu chengine. Mfano;yangu, yake, yako, kwetu n.k
·         Vivumishi Vioneshi:Vivumishi vya aina hii huonyesha mahali au upande kitu kilipo. Vivumishi vya aina hiihujengwa na mzizi {h} kwa vitu vilivyopo karibu na mzizi {le} kwa vitu vilivyo mbali. Mfano; hapa, pale n.k
·         Vivumishi vya kuuliza: Hivi ni vivumishi ambavyo hufafanua nomino kwa kuuliza habari zake. Hujibu swali“gani?ipi? ngapi?”
·         Vivumishi vya pekee:Vivumishi hivi huitwa vya pekee kwa sababu kila kimojawapo huwa na maana maalumu.Pia kila kimojawapo huchukua upatanisho wake wa kisarufi kulingana na ngeli yanomino ambayo kinaivumisha. Mizizi vivumishi hivi niote, o-ote, enye, -enyewe, -ingine, -ingineo. –ote. Huonyesha ujumla wa kitu au vitu-o-oteKivumishi cha aina hii kina maana ya “kila”, “bila kubagua”– enyeKivumishi cha aina hii hutumika kuleta dhanna ya umilikishaji nomino Fulani. –enyeweKivumishi cha aina hii hutumika kuisisitiza nomino fulani.– ingineKivumishi cha aina hii huonyesha/huonesha ‘tofauti na’ au ‘zaidi ya’ kitu Fulani. – ingineoKivumishi cha aina hii hutumika kuonesha/kuonyesha ziadi.
·         Vivumishi vya A- unganifu: Vivumishi vya aina hii huundwa kwa mzizi wa kihusishi a- unganifu. Kihusishi hikihuandamana na nomino kuunda kirai husishi ambacho huvumisha nomino iliyotajwaawali. Vivumishi vya aina hii hutumika kuleta dhanna zifuatazo:--Umilikaji-Nafasi katika orodha. Mfano; wa kwangu, wa Juma, ya tano ya Sita n.k

4. Vielezi
Maana ya vielezi: Vielezi ni maneno yanayofafanua vitenzi, vivumishi auvielezi vyengine. Huweza kuarifu kitendo kilichotendeka kilitendeka wapi , namnagani na hata mara ngapi?

Aina za vielezi
·         Vielezi vya namna au jinsi.Vielezi vya namna hii huonyesha jinsi au namna kitendo kilivyotendeka. Vielezi vyanamna vipo vya aina kadhaa.
- Vielezi vya namna halisi.
Hivi ni vielezi vinavyotumia maneno ambayo kimsingi yana sura ya vielezi moja kwa
moja katika uainishaji wa aina za maneno.Mfano; kuimba sana
-Vielezi vya namna mfanano
Hivi ni vieleziambavyo hutumika kufananisha vitendo na vivumishi au nomino
mbalimbali. Hujengwa kwa kuongeza kiambishi (ki-) au kiambishi (vi-). Viambishi hivi
hujulikana kwa jina la viambishi vya mfanano.Ulifanya vizuri kumsaidia mwanangu.


-Vielezi vya namna vikariri
Hivi nivieleziambavyo hufafanua vitenzi kwa kurudiarudia neno moja mara mbili.Mfano; polepole, harakaharaka.
- Vielezi vya namna hali
Hivi nivieleziambavyo hufafanua juu ya kitendo kilichotendeka kimetendeka katika
hali gani. Mfano; kivivu, kibabe, kizembe, kipole n.k
- Vielezi vya namna ala/kitumizi
Hivi nivielezi vinavyotaja vitu ambavyo hutumika kutendea kitendo. Mfano; kwa kisu, kwa kalamu n.k
- Vielezi vya namna viigizi.
Hivi vinaelezea zaidi jinsi tendo lilivyofanyika kwa kuigiza au kufuatisha sauti
inayojitokeza wakati tendo linapofanyika au kutokea. Mfano; alimpiga paaaah!
·         Vielezi vya idadi. Vielezi vya namna hii huonyesha kuwa kitendo kilitendeka mara fulani au kwa kiasifulani. Mfano; amempiga mara mbili
·         Vielezi vya mahali..Vielezi vya namna hii huonyesha mahali ambapo kitendo kinatokea.Huweza kudokezwakwa viambishi au kwa maneno kamili. Mfano; amekaa jikoni
·         Vielezi vya wakati:Vielezi vya namna hii huonyesha wakati wa kutendeka kwa kitendo.Huweza kutokeakama maneno kamili au hodokezwa kwa kiambishi {po.}Mfano; alimkaribisha alipokuja.

5. VITENZI
Kitenzi ni neno linaloeleza jambo lililotendwa au lililotendeka. Kitenzi huarifu lililofanyika au lililofanywa na kiumbe hai chochote kinachoweza kutenda jambo. Kitenzi cha Kiswahili huundwa na mzizi pamoja na viambishi vyenye uamilifu wa aina tofauti.

                                    AINA ZA VITENZI
·         Vitenzi vikuu (T): Vitenzi vikuu ni vile ambavyo hubeba ujumbemuhimu wa kiarifu cha sentensi. Mfano; Mtoto amekuja.

·         Vitenzi visaidizi: Hivi hutoa taarifa ya kusaidia vitenzi vikuu. Hutoa taarifa kama vile uwezekano , wakati, hali n.k.Vitenzi visaidizi daima hutumika na vitenzi vikuu, ndivyo vinavyobeba viambishi vya wakati. Mfano; Alikua anacheza, Huwa namfurahia.
§  Vitenzi visaidizi huweza kupachikwa urejeshi wa nomino na kusaidia kuifafanua nomino hiyo. Mfano; motto aliyekua anacheza. Virejeshi hivyo ni kama; -ye-, -yo-,    -o-, -lo-, -cho-, -wo- n.k

·         Vitenzi vishirikishi: Hivi ni Vitenzi ambavyo hufanya kazi ya kuunga sehemu mbili za sentensi. Havichukui viambishi vya nafsi, njeo ama hali.Vitenzi vishirikishi ni vya aina mbili, ambavyo nikitenzi kishirikishi “ni” cha uyakinishi na kitenzi shirikishi“si” cha ukanushi.
Kazi za kitenzi kishirikishi
-kushirikisha vipashio vingine katika sentensi
-Kuonesha tabia fulani iliyopo au isiyokuwepo ya mtu fulani au kitu fulani.
-Kuonyesha cheo au kazi anayofanya mtu.
-kuonyesha sifa za mtu.
- kuonyesha umoja wa vitu au watu
-kuonyesha mahali
-kuonyesha umilikishi wa kitu chochote.
                                    6. KIWAKILISHI
Kiwakilishi ni aina ya neno linaloweza kutumika badala ya jina .

            AINA ZA VIWAKILISHI
Viwakilishi vya kuuliza/viwakilishi viulizi ambavyo huashiriwa na mofu / kiambishi {-pi} ambavyo katika tungo hutanguliwa na kiambishi ngeli cha jina husika. Mfano- Mtoto yupi
Wiwakilishi vya urejeshi ambavyo vinajengwa na shina amba pamoja na vipande vidogo vidogo –ye-, -o-, -cho-, vyo, lo, po, mo, ko n.k ambavyo vinachaguliwa kilingana na ngeli ya majina yanayorejeshwa navyo.
Viwakilishi vya idadi: Viwakilishi hivi hutuarifu kuhusu idadi ya nomino hiyo huweza kuwa kamili (halisi) au ya jumla. Mfano; Wengi wamekuja
Viwakilishi vya pekee:-Hivi ni aina ya vivumishi vya pekee kuwakilisha nomino. Hufuata sheria za upatanisho za nomino zinazowakilishwa.
Viwakilishi vya A-unganifu:-Viwakilishi hivi huundwa kwa kihisishi cha A-unganifu kusimamia nominoiliyomilkiwa, inayochukuwa nafasi fulani katika orodha au nomino ya aina fulani.Kihisishi a-unganifu huandamana na nomino kuunda kirai husishi ambacho husimamamahali pa nomino.

                                    7. VIUNGANISHI
Ni maneno, kikundi cha maneno au kiambishi chenye kuunganisha maneno, kirai, kishazi au sentensi.Dhima ya kiunganishi ni kuunga vipashio viwili au zaidi vyenye hadhi sawa kisarufi.

Aina za viunganishi:
·         Viunganishi huru: hivi ni viunganishi vinavyosimama pekee katika tungo, katikati ya vipashio vinavyo ungwa. Hujumuisha: -
-Viunganishi nyongeza/vya kuongeza. Mfano; Tena,Na,Zaidi ya n.k.
- Viunganishi vya sababu/visababishi.  Mfano; Kwa kuwa,kwa sababukwa vile, kutokana na, n.k.
- Viunganishi linganishi/vya kinyume.  Mfano; Ingawa, Japokuwa, Lakini n.k.
- Viunganishi vya wakati.                      Mfano; kasha, baadaye, Halafu, Baada ya n.k.
- Viunganishi vya masharti.                   Mfano; Kama, Ikiwa, Iwapo n.k
- Viunganishi vihusishi                           Mfano; Cha, La, Wa, Za n.k.

·         Viunganishi tegemezi: Ni viambishi ambavyo hutiwa katika kitenzi cha kishazi tegemezi ili kukiunga na kitenzi kikuu cha kishazi huru ambavyo kwa pamoja huunda sentensi changamano au shurtia. Mfano; -ye-, -po-, -ki-, -cho- na -nge-.



8. Vihusishi
Ni maneno ambayo huonyesha uhusiano uliopo baina ya neno moja na jengine.Vihusishi aghlabu huonyesha uhusiano kati ya nomino au kirai nomino na maneno mengine.
Mambo mbalimbali yanayoweza kuonyeshwa na vihusishi
- huonyesha uhusiano wa kiwakati
- huonyesha uhusiano wa mahali
- huonyesha uhusiano wa kulinganisha
- huonyesha uhusiano wa umilikaji
- huonyesha uhusiano wa sababu/kiini
 Aina za vihusishi
-vihusishi vya wakatiMfano; kabla ya, baada ya n.k
-vihusishi vya mahaliMfano; chini ya, juu ya, ndani ya, mbele ya n.k.
- vihusishi vya ulinganishi/ vya kulinganisha Mfano; kuliko, zaidi ya n.k.
-vihusishi vya sababu/ kusudi/nia Mfano; kwa sababu ya, kwa ajili ya n.k.
-vihusishi vya ala (kifaa)-Mfano; kwa
- vihusishi vimilikishi Mfano; cha, za n.k.
-vihusishi vya namna/jinsi/hali Mfano; moto wa kuotea mbali, macho ya mviringo
Matumizi ya ziada ya kihusishi “kwa”
-kihusishi hiki huonyesha mahali au upande
-kihusishi hiki huonyesha sababu au kisababishi cha jambo
-kihusishi hiki huonyesha wakati
-kihusishi hiki huonyesha sehemu Fulani ya kitu kikubwa
-kihusishi hiki hutumika kuonyesha ‘nia ya pamoja na’

-Kihusishi hiki huonyesha jinsi kitendo kilivyotendeka


Anapatikana kupitia:
SIMU - +255 765 304 501
BARUA PEPE  – yusuphpius19@gmail.com
UKURAHAMA / FACEBOOK AC – Yusuph Pius Mtz Huru
UKURASA WA UKURAHAMA – Teaching Advancement
TWITTER – YUSUPH PIUS.

Hakuna maoni: