Jumamosi, 15 Machi 2014

SARUFI KISWAHILI 4

UCHANGANUZI WA SENTENSI
Tunapoitenga sentensi katika makundi mbalimbali yanayoiunda sentensi hiyo kutoka kundi kubwa hadi dogo kabisa la leksia (neno), hali hiyo ndiyo inayojulikana kama kuchanganua sentensi. Kuchanganua ni kutolea ufafanuzi wa kitu kwa kukielezea kwa mgawanyo wake. Uchanganuzi wa sentensi hupitia hatua zifuatazo:-
                               I.            Kuiainisha sentensi hiyo. Hapa sentensi hutambulishwa kuwa ni aina gani.
                            II.            Kutenga sentensi hiyo katika sehemu zake mbili zinazoiunda, yaani kiima na kiarifu.
                         III.            Kutambulisha makundi ya maneno yanayopatikana katika sehemu hizo.
                         IV.            Kubainisha aina za maneno yanayounda makundi hayo ya maneno.
                            V.            Kuiandika sentensi hiyo kwa kufuatisha aina zake za maneno.
Ipo pia mikabala miwili ya uchanganuzi wa sentensi ambapo yote hufuata hatua zilezile lakini tofauti inayojitokeza ni matumizi ya istilahi za virai upande wa kiarifu.
A)  Mkabala wa kikazi / kimapokeo. Huu hutenga sentensi katika kiima na kiarifu pia hutumia istilahi; Chagizo badala ya Kirai kielezi (KE), Shamirisho badala ya Kirai nomino (KN), na Prediketa badala ya Kirai kitenzi (KT) ila ni katika upande wa kiarifu.
B)  Mkabala wa kimuundo / kisasa. Huu hutenga sentensi katika Kundi nomino na Kundi kitenz na pia hutumia istilahi za kawaida za virai.













NJIA ZA UCHANGANUZI WA SENTENSI
A.    Njia ya matawi / ngowe (mkabala wa kimuundo).
Mfano.

i.                    Mtoto mzuri amenunuliwa zawadi.

S. Sahili.
    
                       

KN                                                                              KT

N                     V                                                         T                                  E


Mtoto              Mzuri                                       amenunuliwa                           zawadi

Mkabala wa kikazi.

S. Sahili.
    
                        K                                 A

                                                            T                      Ch

                    N                     V                                                    E

                                                                                                                       
             Mtoto                   Mzuri            amenunuliwa            zawadi


ii.                  Mwanafunzi aliyefaulu amehama kimyakimya.
Kimuundo
                                                            S. Changamano

                                                KN                                   KT

                        N                                 βV                                                                  

                                                            Ts                    T                                        E
           
Mwanafunzi                              aliyefaulu      amehama                     Kimyakimya
                                                     
                    Kikazi

S. Changamano

                                                K                                      A

                        N                                 βV                   Pr                     Ch

                                                            Ts                    T                                  E
           
Mwanafunzi                               aliyefaulu              amehama                        Kimyakimya








iii.                Mama anapika na Baba anasoma gazeti.
Kimuundo
                                                      S. Ambatano
          
                                          S1                                       S2

                  KN                              KT     U     KN                  KT

              N                                     T                   N                  T                      E
         
  Mama                            anapika           na     Baba                anasoma          gazeti

                  Kikazi
                                                      S. Ambatano
          
                                          S1                                       S2
                              K                     A      U      K                     A

                  N                                 T                N                     T                      Ch

                                                                                                                        E
         
       Mama                             anapika      na    Baba           anasoma            gazeti








B.     Njia ya maelezo.
Kimuundo.
   Mfano; i. Mtoto mfupi anataka chai.
Hii ni sentensi sahili.
Sentensi sahili hii ina Kirai nomino na kirai kitenzi.
Kirai nomino kimeundwa na Nomino na Kivumishi.
Nomino ni ‘Mtoto’.
Kivumishi ni ‘Mzuri’.
Kirai kitenzi kimeundwa na kitenzi kikuu na kirai nomino.
Kitenzi kikuu ni ‘Anataka’.
Kirai nomino hicho kimeundwa na Jina.
Jina hilo ni ‘Chai’.
Kikazi
Hii ni sentensi sahili.
Sentensi hii imeundwa na Kiima na Kiarifu.
Kiima  kina Jina na Kivumishi.
Jina hilo ni ‘Mtoto’.
Kivumishi hicho ni ‘Mzuri’.
Kiarifu kimeundwa na Kitenzi kikuu na Shamirisho.
Kitenzi kikuu ni ‘Anataka’.
Shamirisho ni ‘Chai’.
ii.                  Mama aliyenipenda ameniletea zawadi cha ajabu Mama yangu amechukia.
Kimuundo.
Sentensi hii ni ambatano.
Sentensi hii ina sentensi mbili zinazounganishwa na kiunganishi.
Sentensi ya kwanza ina Kirai nomino na kirai kitenzi.
Kirai nomino kimeunda na Jina na kishazi tegemezi kivumishi.
Jina ni ‘Mama’.
Kishazi tegemezi kivumishi hicho ni kitenzi kisaidizi.
Kitenzi kisaidizi hicho ni ‘Aliyenipenda’.
Kirai kitenzi kimeundwa na kitenzi kikuu na Jina.
Kitenzi kikuu ni ‘Ameniletea’.
Jina ni ‘zawadi’
Kiunganishi ni ‘Cha ajabu’
Sentensi ya pili imeundwa na kirai nomino na kirai kitenzi.
Kirai nomino hicho kimendwa na Jina na kivumishi.
Jina ni ‘Mama’.
Kivumishi ni ‘yangu’.
Kirai kielezi kimeundwa na kitenzi kikuu.
Kitenzi hicho ni ‘amechukia’.
      Kikazi
Sentensi hii ni ambatano.
Sentensi hii ina sentensi mbili zinazounganishwa na kiunganishi.
Sentensi ya kwanza ina Kiima na Kiarifu.
Kiima kimeundwa na Jina na kishazi tegemezi kivumishi.
Jina ni ‘Mama’.
Kishazi tegemezi kivumishi hicho ni kitenzi kisaidizi.
Kitenzi kisaidizi hicho ni ‘Aliyenipenda’.
Kiarifu kimeundwa na kitenzi kikuu na Shamirisho.
Kitenzi kikuu ni ‘Ameniletea’.
Shamirisho ni ‘zawadi’
Kiunganishi ni ‘Cha ajabu’
Sentensi ya pili imeundwa na kiima na Kiarifu.
Kiima kimendwa na Jina na kivumishi.
Jina ni ‘Mama’.
Kivumishi ni ‘yangu’.
Kiarifu kimeunda na Prediketa.
Prediketa hiyo ni ‘amechukia’.




C.    Njia yamshale au Mstari
Mfano.  Mkamwana wake aliyemzalia mwanae watoto amepata matatizo lakini hakwenda kumuona.
            Kimuundo
S                                 Ambatano
S                                  S1 + U +S2
S1                                                 KN + KT
KN                               N + V + βV
N                                  Mkamwana
V                                   Wake
βV                                Ts + V + N
Ts                                 Aliyemzalia
V                                  Mwanae
N                                  Watoto
KT                                T + KN
T                                   Amepata
KN                                N
N                                  Matatizo
U                                  Lakini
S2                                                  KN +KT
KN                                θ
KT                                 Ts + T
TS                                  Hakwenda
T                                    Kumuona







             Kikazi
S                                 Ambatano
S                                  S1 + U +S2
S1                                                K + A
K                                  N + V + βV
N                                  Mkamwana
V                                  Wake
βV                                Ts + V + N
Ts                                 Aliyemzalia
V                                  Mwanae
N                                  Watoto
A                                   Pr + Sh
Pr                                   Amepata
Sh                                N
N                                  Matatizo
U                                  Lakini
S2                                                  K +A
K                                  θ
A                                 Pr
Pr                                 T + Tj
TS                                  Hakwenda
Tj                                    Kumuona









D.    Njia ya visanduku
Mfano; Kijana aliyemleta ameondoka na mtoto haonekani.
      Kimuundo
                                                 S. Ambatano
                   S1
U
                        S2
        KN
         KT

     KN
      KT
N
βV
         T
U
     N
     T
Kijana
aliyemleta
ameondoka
na
mtoto
haonekani
     N
   TS
       T
U
      N
      T


Kikazi
                                                 S. Ambatano
                   S1
U
                        S2
        K
         A

     K
      A
N
βV
         Pr
U
     N
     Pr
Kijana
aliyemleta
ameondoka
na
mtoto
haonekani
    N
      TS
          T
U
      N
       T








Mfano 2. Mwalimu aliyefukuzwa jana shuleni amerudi kwao.
           Kimuundo
                                                                          S. Changamano
                      KN
                          KT
        N
                       βV
              T
           E
Mwalimu
aliyefukuzwa
jana
shuleni
amerudi
kwao
        N
      Ts
 E1
E2
      T
    E


              Kikazi
                                                                          S. Changamano
                      K
                          A
        N
                       βV
              Pr
           Ch
Mwalimu
aliyefukuzwa
jana
shuleni
amerudi
kwao
        N
      Ts
 E1
E2
      T
    E











ZOEZI
1.      ‘Kila sentensi ni tungo ila si kila tungo ni bsentensi’. Thibitisha kwa mifano ya kutosha.
2.      Kwa mifano eleza maana ya istilahi zifuatazo:-
a.       Kiima
b.      Kiarifu
c.       Yambwa
d.      Shamirisho
e.       Chagizo
f.       Sentensi
g.      Sentensi shurutia
3.      Kwa mifano fafanua miundo tofautitofauti ya aina zifuatazo za sentensi.
a.       Sentensi sahili
b.      Sentensi shurutia
c.       Sentensi ambatano
d.      Sentensi changamano
4.      Taja vipashio vya:-
a.       Kiima
b.      Kiarifu
5.      Bainisha mikabala na hatua za kufuatwa katika kuchanganua sentensi.
6.      Changanua sentensi hii kwa kutumia mikabala yote miwili kwa njia ya Ngowe:
-          Mwanafunzi aliyehitimu amefaulu na amewafurahisha wazazi wake.
7.      Changanua sentensi zifuatazo kwa kufuata maelekezo katika mabano.
-          Mtoto amefariki. (Ngowe – Kimuundo)
-          Mtoto amefika ila aliyemleta hafahamiki. (Mshale – Kikazi)
-          Angelijua, angelisoma kwa kuwa hakusoma ameshindwa mtihani. ( Jedwali – kimuundo na kikazi).
-          Mtu akifa anazikwa lakini Ng’ombe akifa anatupwa. ( Maelezo- kimuundo).




                               NGELI ZA NOMINO
    Ni namna ya kuweka majina katika makundi yanayofanana. Majina ya Kiswahili yanaweza kuwekwa katika makundi mbalimbali. Makundi hayo yamegawa na wanaisimu ya Kiswahili kwa kuzingatia maumbo ya alomofu za umoja na uwingi wa majina (kimofolojia) na kwa kuzingatia namna majina yanavyopatana na viambishi awali vya vitenzi (upatanisho wa kisarufi / kisintaksia).
1.      Kimofolojia: Katika kigezo hiki wanaisimu wameyapanga majina kulingana na alomofu za umoja na uwingi za majina hayo. Huu ni mtazamo mkongwe ambao uliofuatwa na wanasarufi wa kimapokeo wakiongozwa na Meinholf, Broomfield na Ashton mnamo miaka ya 1920 – 50. Uchambuzi ulikua kama ifuatavyo:-
1.      M-
2.      WA-
i). Majina ya viumbe vyenye uhai
ispokuwa mimea. Mfano; Mtoto – Watoto, Mzee – Wazee, Mkurya - Wakurya
ii) Majina yanayotokana na vitenzi
vinavyotaja watu. Mfano; Msomi – Wasomi, Mkulima – Wakulima, Mfanyakazi – Wafanyakazi.
3.     M-
4.      MI-
i). Majina ya mimea. Mfano; Mti – Miti, Mwembe, Miembe, Mpera – Mipera.
ii) Majina ya vitu yanayoanza na M- Mfano; Mto – Mito, Msumari – Misumari.
5.      KI-
6.      VI-
i). Majina ya vitu yanayoanza na ki- (umoja) na vi- (wingi). Mfano; Kiti – Viti, Kisu – Visu, Kikapu – Vikapu.
ii). Majina ya viumbe yanayoambishwa na ch- umoja na vy-uwingi. Mfano; Chura – Vyura, Chakula – Vyakula, Chuma – Vyuma.
7.      JI-
8.      MA-
i). Majina yanayoanza na ji- umoja na ma- uwingi. Mfano; Jicho – Macho, Jini – Majini, Jiwe – Mawe, Jina – Majina.
ii). Majina ya mkopo yenye ma- (wingi). Mfano; Bwana – Mabwana, Shati – Mashati.
iii). Majina yenye kueleza dhanna ya wingi japokuwa hayahesabiki. Maji, Majani, Maua, Maini.
9.      N-
i). Majina ambayo huanza na N inayofuatwa na konsonanti, ch-, d-,
g-, j-, z-, na y- katika umoja na wingi. Mfano; Nchi, Ndama, Ngoma, Njaa, Nzi, Nyasi.
ii). Majina yanayoanza na mb-, mv. Mfano; Mbwa, Mvi.
iii). Majina ya mkopo. Mfano; Taa, redio, Kompyuta, Kalamu.
10.  U-
11.  N-
i). Majina yote yanayoanza na U umoja na N-, mb (wingi). Mfano; Ubao – Mbao, Ulimi – Ndimi, Uso – Nyuso.
12.  U-
13.  MA-
i). Majina yote yanayoanza na uumoja na ma- wingi. Mfano; Uasi – Maasi, Uchweo – Machweo, Ugonjwa – Magonjwa.
14.  KU-
i). Majina yanayotokana na vitenzi yanayoanza na ku- (vitenzi-jina). Mfano; kucheza, Kulima, Kuimba, Kupenda.
15.  PA-

i). Huonesha mahali hasa. Mfano; Pale
16.  MU-
i). Huonesha mahali pa ndani. Mfano; Mule
17.  KU
i). Huonesha mahali pa mbali, pakubwa zaidi au popote. Mfano; Kule

UBORA WA KIGEZO CHA KIMOFOLOJIA
                   I.            Uwezekano wa kuzigawa nomino nyingi za Kiswahili ni mkubwa kwa kuwa nyingi zimegawanyika katika maumbo hayo ya umojha na uwingi.
                II.            Ni kigezo muhimu kwani kinajikita zaidi katika nomino na kivumishi chake peke yake hakigusi aina nyingine ya neno tofauti na kigeso cha kisintaksia ambacho hugusa hadi kitenzi.
             III.            Huwasaidia wanasarufi linganishi kuonesha uhusiano wa lugha za vikoa kimoja.

        UPUNGUFU WA KIGEZO HIKI.
                               I.            Kuna viambishi katika ngeli tofauti vinavyofanana. Mfano Kiambishi M- kinajitokeza katika ngeli ya 1 na 3 na MA- inajitokeza katika ngeli ya 8 na 13.
                            II.            Kuna nomino nyingine ambazo hazijidhihirishi katika umoja na uwingi. Mfano ngeli ya 8 na 9.
2.      Kigezo cha sintaksia /upatanisho wa kisarufi:
   Huu ni mtazamo wa kisasa wa uainishaji wa ngeli ambao umeyagawa majina katika makundi kulingana na upatanisho wa kisarufi kat ya jina na viambishi awali vilivyo katika vitenzi. Kwa mujibu wa mtazamo huu, majina yamepangwa katika makundi tisa ambayo ni:-
1.      A -WA
Mfano; Mtoto anacheza / Watoto wanacheza.
            Mzee analima / Wazee wanalima.
             Mwanafunzi anasoma / Wanafunzi wanasoma.
2.      U – I
Mfano; Mkufu umekatika / Mikufu imekatika.
             Mji umevamiwa / Miji imevamiwa.
             Mkaa umemwagika / Mikaa imemwagika.
3.      LI – YA
Mfano; Gogo limevunjika / Magogo yamevunjika.
             Gari limepotea / Magari yamepotea.
              Jiko limewaka / Majiko yamewaka
4.      KI – VI
Mfano;   Kiapo kimekiukwa / Viapo vimekiukwa.
               Kilima kimesawazishwa / Vilima vimesawazishwa.
               Kikongwe kimeuawa / Vikongwe vimeuawa.
5.      I – ZI
Mfano; Ng’ombe imechinjwa / Ng’ombe zimechinjwa.
             Nguo imechanika / Nguo zimechanika.
              Nchi imekosa amani / Nchi zimekosa amani.
6.      U – ZI
Mfano; Ubao umeandikika / Mbao zimeandikika.
             Ukuta umeanguka / Kuta zimeanguka.
             Uzi umetumika / Nyuzi zimetumika.
7.      U – YA
Mfano; Ugonjwa unatisha / Magonjwa yanatisha.
             Uasi umekithiri / Maasi yamekithiri.
8.      KU
Mfano; Kulima kunachosha.
             Kuimba kwake kunafurahisha.
           Kufurahi kwake kumemponya.
9.      PA – MU - KU
Mfano; Hapa pananuka.
             Humu mna nzi.
             Kule kumebomoka.
UBORA WA KIGEZO CHA KISINTAKSIA
n  Unajitosheleza kwa kuwa kila jina inakuwa na upatanishi wake katika kitenzi.
UPUNGUFU WA KIGEZO HIKI
I.                   Kuna viambishi vinavyojirudia. Mfano, U- kimejitokeza katika ngeli ya 2, 6 na 7.
II.                Huyaweka majina yenye maumbo tofauti katika ngeli moja.
III.             Kunaweza kuwa na utata katika upatanisho kwa baadhi ya majina kama “makala”
      Mfano; Makala yamechapishwa.
                  Makala imechapishwa.
Sentensi hizo zote zinatumika ila hatuna wingi wa makala katika Kiswahili.

ZOEZI
1.      Eleza dhana zifuatazo kwa makini:-
a.       Ngeli za majina
b.      Ngeli za majina kimofolojia
c.       Upatanisho wa kisarufi
2.      Yapange majina yafuatayo kwa kigezo cha sarufi mapokeo:- Nazi, Chungwa, Mtu, Mchanga, Ukuta, Ulimi, Uovu, Chapati, Maliwato, Pale, Panga, Kisima, Godoro, Nhi, Mchungwa.
3.      Fafanua faida na hasara za kila mkabalka wa uainishaji wa ngeli za majina.
4.      Onesha mpangilio wa ngeli za majina kisintaksia kisha uoneshe mapungu yake.










                  NJIA ZA UUNZI WA MISAMIATI
            Msamiati ni jumla ya maneno yanayopatikana katika lugha. Uundaji wa maneno mapya ni ujuzi ulioanza tangu awali mwanadamu alipoipata lugha ili kuiwezesha lugha yake kuwa toshelevu na endelevu. Uundaji wa maneno huja mara baada ya kuwepo kwa vitu vipya mwanadamu anavyokutana navyo katika mazingira yake.
            Kwa nini tuunde maneno mapya?
·         Kuwezesha matumizi ya kawaida yanayobadilika kila siku.
·         Kuwezesha kukua kwa taaluma ya utafsiri.
·         Kupata msamiati kubalifu katika muktadha mahsusi.
·         Kukuza utamaduni wa jamii.
·         Kukidhi haja ya kitaaluma / kielimu.
Njia za uundaji wa maneno.
                               I.            Uradidi, katika njia hii neno au silabi huweza kurudiwa rudiwa ili kupata maneno mapya katika lugha. Neno lote linaporudiwa tunapata urudufu kamili, lakini tukirudia sehemu ya neno tunaita urudufu nusu.
Mfano; polepole, harakaharaka, kizunguzungu, kiwiliwili.
                            II.            Kufupisha maneno, ufupisha hutokea pale tunapochukua herufi za mwanzo za maneno hayo. Kuna aina mbili za ufupisho wa maneno:-
a.       Akronimi ni ufupisho wa kuchukua herufi za mwanzoni mwa maneno tu. Mfano; UKIMWI – Upungufu wa Kinga Mwilini.
CHANETA – Chama cha Netiboli Tanzania.
                                                            TUKI – Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili.
b.      Uhulutishaji (blending) ni ufupisho wa kuweka pamoja vijisehemu vya maneno kuunda neno jipya.
Mfano; Msikwao – Mtu asiye na kwao.
            Joto baridi – Jotoridi
            Mnyama mfu – Nyamafu
                         III.            Kufananisha sauti, baadhi ya maneno ya Kiswahili yametokana na uwigaji wa sauti au dhana ya kitu Fulani.
Mfano; Pikipiki – Limetokana na mlio wa chombo hicho.
Kifaru – zana ya kivita, umbo lake linafanana na kifaru    mnyama.
                         IV.            Kuambatanisha maneno, hapa maneno mawili tofauti hushikamanishwa na kuwa neno moja lenye maana tofauti na ile ya kwanza. Mfano; Mwanakwetu, Mcheza kwao, Mwananchi, Mwanachama, Mfamaji, Mpigambizi n.k.
                            V.            Kutohoa maneno, ni mchakato wa kuhamisha maneno kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine na kuyatumia jinsi yalivyo huku yakibadilishwa kuwaq na muundo wa maneno ya lugha hiyo. Kiswahili kimetohoa maneno kutoka lugha mbalimbali kama;
a.      kiingereza maneno kama; shati, baiskeli, kompyuta, trekta, waya, redio n.k.
b.      Kiajemi maneno kama; bafta, kodi, darubini, jemedari, rosheni, randa n.k.
c.       Kihindi maneno kama; kanuni, achali, gari, bajia, bima, tumbaku, dobi n.k.
d.      Kiarabu maneno kama; hisani, salama, shukurani, daima, elimu, kauli, fahamu, mahabusu, ila, kulaki n.k.
e.       Kireno maneno kama; meza, mvinyo, seti, korosho, leso, kopa, roda, dama n.k.

ZOEZI
1.      Eleza njia zilizotumika katika kuunda maneno haya ya Kiswahili.
a.       Kiherehere
b.      Mtukwao
c.       Simu ya mkononi
d.      Baiskeli
e.       UKUTA
f.       Mkono wa tembo
g.      Kifaru









                                    WASIFU WA MWANDISHI
Yusuph P Mhindi, alizaliwa miaka 25 iliyopita mjini Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara. Akiwa na miaka saba baada ya kuzaliwa alianza masomo ya elimu ya msingi katika shule ya msingi Mapinduzi iliyoko Mjini Mugumu wilayani Serengeti – Mara.
Alipohitimu elimu ya msingi, alifanikiwa kujiendeleza na Elimu ya sekondari ambapo alisoma Machochwe Shule ya Upili, Bwasi Shule ya Upili na hatimaye safari yake ya Elimu ya Sekondari ilitamatika akiwa Nyansincha Sekondari huko Mara Tanzania.
Hakuishia hapo alijiimarisha zaidi kielimu baada ya kujiunga na Elimu ya Kidato cha tano na sita kwa mchepuo wa sanaa masomo ya Historia, Kiingereza na Kiswahili katika Shule ya Upili Kibara. Na rehema za Mwenyezi Mungu zikizidi kuwa tunu kwake kwani alifaulu pia.
Alijiunga na Chuo Kikuu cha Mt. Augustino kilichopo Jijini Mwanza kwa Shahada ya Sanaa na Elimu, akiwa amejikita katika masomo ya lugha yaani Kiswahili na Kiingereza nakufanikiwa kufanya utafiti juu ya ‘Athari za Kazi za Wazazi kwa Machaguzi ya Kazi kwa Watoto.’  Alihitimu masomo hayo mwaka  2013.
Ameshawahi kuwa mwalimu wa kujitolea katika shule kadhaa zikiwemo Chitengule Sekondari, Kabasa Sekondari, Nyakurunduma Sekondari, Imani Sekondari na kote huko amekuwa akifundisha zaidi somo la Kiswahili na Kiingereza na sasa ameajiliwa kwa muda katika Taasisi ya Elimu Emarx iliyopo mjini Dodoma kama mwalimu wa somo la Kiswahili.
Hii ni chapa yake ya kwanza kama Kitini na anajitayarisha kufanya mapinduzi katika tasnia ya uandishi wa vitabu vya Taaluma na hata vya kijamii pia.
Mungu mbariki Yusuph P Mhindi, ibariki sekta ya Elimu Tanzania, ibariki Tanzania na bara zima la Afrika.


Anapatikana kupitia:
SIMU - +255 765 304 501
BARUA PEPE  – yusuphpius19@gmail.com
UKURAHAMA / FACEBOOK AC – Yusuph Pius Mtz Huru
UKURASA WA UKURAHAMA – Teaching Advancement

TWITTER – YUSUPH PIUS.